12. Juu ya kabila la Benyamini alisema:“Hili ni kabila alipendalo Mwenyezi-Mungu,nalo hukaa salama karibu naye.Yeye hulilinda mchana kutwa,na kukaa kati ya milima yake.”
13. Juu ya kabila la Yosefu alisema:“Mwenyezi-Mungu na aibariki nchi yake,kwa baraka nzuri kabisa kutoka juu,
14. ibarikiwe kwa matunda bora yalioiva kwa jua,kwa matunda ya kila mwezi;
15. kwa mazao bora ya milima ya kale,na mazao tele ya milima ya kale,
16. Nchi yake ijae yote yaliyo mema,ibarikiwe kwa wema wa Mwenyezi-Mungu,ambaye alitokea katika kichaka.Baraka hizi ziwashukie watu wa kabila la Yosefu,aliyekuwa mkuu miongoni mwa ndugu zake.