Kumbukumbu La Sheria 33:12-16 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Juu ya kabila la Benyamini alisema:“Hili ni kabila alipendalo Mwenyezi-Mungu,nalo hukaa salama karibu naye.Yeye hulilinda mchana kutwa,na kukaa kati ya milima yake.”

13. Juu ya kabila la Yosefu alisema:“Mwenyezi-Mungu na aibariki nchi yake,kwa baraka nzuri kabisa kutoka juu,

14. ibarikiwe kwa matunda bora yalioiva kwa jua,kwa matunda ya kila mwezi;

15. kwa mazao bora ya milima ya kale,na mazao tele ya milima ya kale,

16. Nchi yake ijae yote yaliyo mema,ibarikiwe kwa wema wa Mwenyezi-Mungu,ambaye alitokea katika kichaka.Baraka hizi ziwashukie watu wa kabila la Yosefu,aliyekuwa mkuu miongoni mwa ndugu zake.

Kumbukumbu La Sheria 33