Kumbukumbu La Sheria 28:13-18 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atawafanya kuwa wa kwanza kwa nguvu na sio wa mwisho. Mtaendelea mbele na sio kurudi nyuma kama mkishika amri zake ambazo ninawapeni leo na kuwa waangalifu kuzitekeleza,

14. bila kugeuka kulia au kushoto kuifuata miungu mingine na kuitumikia.

15. “Lakini kama hamtaitii sauti ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, au msipokuwa waangalifu kutekeleza amri zake zote na masharti ninayowaamuru leo, basi mtapatwa na laana hizi zote:

16. Mtapata laana katika miji yenu na mashamba yenu.

17. Vikapu vyenu vya nafaka vitalaaniwa na vyombo vyenu vya kukandia mkate.

18. Watoto wenu watalaaniwa na mazao yenu ya nchi; mifugo yenu italaaniwa isiongezeke.

Kumbukumbu La Sheria 28