10. “Ukimkopesha jirani kitu chochote, usiingie kwake kuchukua rehani.
11. Msubiri nje na umwache yeye mwenyewe akuletee hiyo rehani.
12. Kama yeye ni maskini usikae na rehani hiyo usiku kucha.
13. Mrudishie kila siku jioni ili usiku aweze kujifunika na kukutakia baraka. Kufanya hivyo ni jambo la uadilifu mbele ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.
14. “Usimdhulumu kibarua maskini na mhitaji, awe Mwisraeli au mmoja wa wageni wanaoishi katika miji yenu.