16. bundi, mumbi, bundi mkubwa,
17. mwari, nderi, mnandi,
18. membe, koikoi kwa aina zake, hudihudi na popo.
19. Na wadudu wote wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.
20. Mnaweza kula viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi.
21. Msile nyamafu yoyote; mnaweza kumpa mgeni anayeishi katika miji yenu, ale, au mnaweza kumwuzia mtu wa taifa lingine, kwa sababu nyinyi ni watakatifu na Mwenyezi-Mungu ni Mungu wenu. Msimchemshe mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.
22. “Toeni sehemu moja ya kumi ya mazao yenu yote ya shambani kila mwaka.