5. Viatu vyote vya washambulizi vitanina mavazi yote yenye madoa ya damuyatateketezwa kama kuni za kuwasha moto.
6. Maana mtoto amezaliwa kwa ajili yetu,tumepewa mtoto wa kiume.Naye atapewa mamlaka ya kutawala.Ataitwa: “Mshauri wa Ajabu”.“Mungu Mwenye Nguvu”,“Baba wa Milele”,“Mfalme wa Amani”.
7. Utawala wake utastawi daima,amani ya ufalme wake haitakoma.Atachukua wadhifa wa mfalme Daudina kutawala juu ya ufalme wake;ataustawisha na kuuimarisha,kwa haki na uadilifu,tangu sasa na hata milele.Hayo atayafanya Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
8. Mwenyezi-Mungu ametoa tamko dhidi ya Yakobonalo litampata Israeli.
9. Watu wote watatambua,ukoo wote wa Efraimuna wakazi wa Samaria.Kwa kiburi na majivuno wanasema:
10. “Kuta za matofali zimeangukalakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa!Nyumba za boriti za mikuyu zimeharibiwalakini mahali pake tutajenga za mierezi.”
11. Basi, Mwenyezi-Mungu atawaletea wapinzanina kuwachochea maadui zao.
12. Waaramu upande wa mashariki,Wafilisti upande wa magharibi,wamepanua vinywa vyao kuimeza Israeli.Hata hivyo, hasira yake haijatulia,bado ameunyosha mkono wake.
13. Ingawa aliwaadhibu watu,hawakumrudia Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
14. Basi kwa muda wa siku moja tu,Mwenyezi-Mungu atakata katika Israeli vichwa na mikia,tawi la mtende na nyasi: