10. Wakazi wa Yerusalemu, tokeni, tokeni nje ya mji,watayarishieni njia watu wenu wanaorejea!Jengeni! Jengeni barabara na kuondoa mawe yote!Wekeni alama kwa ajili ya watu.
11. Mwenyezi-Mungu ametangaza duniani kote,waambie watu wa Siyoni:“Mkombozi wenu anakuja,zawadi yake iko pamoja nayena tuzo lake liko mbele yake.”
12. Nyinyi mtaitwa: “Watu Watakatifu”,“Watu waliokombolewa na Mwenyezi-Mungu.”Na Yerusalemu utaitwa: “Mji aupendao Mungu”,“Mji ambao Mungu hakuuacha.”