5. Utaona na uso wako utangara,moyo wako utasisimka na kushangilia.Maana utajiri wa bahari utakutiririkia,mali za mataifa zitaletwa kwako.
6. Makundi ya ngamia yataifunika nchi yako,naam, ndama wa ngamia kutoka Midiani na Efa;wote kutoka Sheba watakuja.Watakuletea dhahabu na ubani,wakitangaza sifa za Mwenyezi-Mungu.
7. Makundi ya kondoo wa Kedari yatakusanywa kwako,utaweza kuwatumia kondoo madume wa Nebayothi kuwa kafara;utawatoa kuwa tambiko inayokubalika madhabahuni pa Mungu,naye ataitukuza nyumba yake tukufu.