12. Magofu yenu ya kale yatajengwa;mtajenga upya juu ya misingi iliyoachwa zamani.Nanyi mtaitwa watu waliotengeneza upya kuta,watu waliozifanya barabara za mji zipitike tena.
13. “Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato,ukaacha shughuli zako siku yangu hiyo takatifu;kama ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha,ukaiheshimu siku hiyo takatifu ya Mwenyezi-Mungu,ukaacha na shughuli zako na kupiga domo,
14. utapata furaha yako kwangu mimi Mwenyezi-Mungu,nitakupatia ushindi katika kila pingamizi nchini,nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako.Mimi, Mwenyezi-Mungu, nimesema.”