4. Maana mimi Mwenyezi-Mungu nasema:Towashi ashikaye sheria zangu za Sabato,anayefanya mambo yanayonipendeza,na kulizingatia agano langu,
5. nitampa nafasi maalumu na ya sifakatika nyumba yangu na kuta zake;nafasi bora kuliko kuwa na watoto wa kiume na wa kike:Nitampa jina la kukumbukwa daima,na ambalo halitafutwa kamwe.
6. “Watu wageni watakaonikiri mimi Mwenyezi-Mungu,watakaoniheshimu, wakapenda jina langu na kuwa watumishi wangu,wote watakaoshika Sabato bila kuikufuru,watu watakaozingatia agano langu,
7. hao nitawaleta katika mlima wangu mtakatifu,na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala;tambiko na sadaka zao zitakubaliwa madhabahuni pangu.Maana nyumba yangu itaitwa:‘Nyumba ya sala kwa ajili ya watu wote’.