1. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Nisikilizeni enyi mnaotaka kukombolewa,nyinyi mnaonitafuta mimi Mwenyezi-Mungu.Utazameni mwamba mlimochongwa,chimbo la mawe mlimochimbuliwa.
2. Mkumbukeni Abrahamu babu yenu,na Sara aliyewazaa nyinyi.Abrahamu alikuwa hana mtoto wakati nilipomwita,lakini nilimbariki na kumfanya kuwa na wengi.
3. “Mimi Mwenyezi-Mungu nitaufariji mji wa Siyoni,nitaparekebisha mahali pake pote palipoharibika.Nyika zake nitazifanya kama bustani ya Edeni,majangwa yake kama bustani ya Mwenyezi-Mungu.Kwake kutapatikana furaha na shangwe,na nyimbo za shukrani zitasikika humo.
4. “Nisikilizeni enyi watu wangu,nitegeeni sikio enyi taifa langu.Sheria na haki zitatoka kwangu mimi;nazo zitakuwa mwanga wa mataifa.
5. Nitaleta ukombozi hima;wokovu nitakaoleta waanza kutokea.Mimi mwenyewe nitayatawala mataifa.Wakazi wa nchi za mbali wananingojea,wanaitegemea nguvu yangu.