1. Nitaimba juu ya rafiki yangu,wimbo wa rafiki yangu na shamba lake la mizabibu:Rafiki yangu alikuwa na shamba la mizabibujuu ya kilima chenye rutuba nyingi.
2. Alililima vizuri na kuondoa mawe yote,akaotesha humo mizabibu iliyochaguliwa;alijenga mnara wa ulinzi katikati yake,akachimba kisima cha kusindikia divai.Kisha akangojea lizae zabibu,lakini likazaa zabibu chungu.
3. Kwa hiyo rafiki yangu anasema hivi:“Enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda,amueni tafadhali kati yangu na shamba langu.