6. ili watu wote, toka mashariki hadi magharibi,wajue kwamba hakuna Mungu mwingine ila mimi;mimi ni Mwenyezi-Mungu na hakuna mwingine.
7. Mimi hufanya mwanga na kuumba giza;huleta fanaka na kusababisha balaa.Mimi Mwenyezi-Mungu hutenda vitu hivi vyote.
8. Enyi mbingu, nyesheni kutoka huko juu,mawingu na yadondoshe uadilifu;dunia na ifunuke, ichipushe wokovu,na kuchanusha uadilifu pia!Mimi, Mwenyezi-Mungu nimefanya hayo.”
9. Ole wake mtu ashindanaye na Muumba wake,mtu aliye chombo cha udongokushindana na mfinyanzi wake!Je, udongo humwuliza anayeufinyanga:“Unatengeneza nini hapa?”Au kumwambia, “Kazi yako si kamili!”