26. Lakini huuthibitisha ujumbe wa mtumishi wangu,na kukamilisha maaguzi ya wajumbe wangu.Mimi ndimi niuambiaye mji wa Yerusalemu:Wewe Yerusalemu, utakaliwa tena na watu.Na miji ya Yuda:Nyinyi mtajengeka tena:Magofu yenu nitayarekebisha tena.
27. Mimi ndimi ninayeviamuru vilindi:Kaukeni.
28. Ndimi nimwambiaye Koreshi:Wewe utawachunga watu kwa niaba yangu.Wewe utatekeleza mipango yangu yote.Ndimi ninayesema kuhusu Yerusalemu:Wewe Yerusalemu utajengwa tena upya;na juu ya hekalu: Msingi wako utawekwa tena.”