Isaya 44:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Sikiliza ewe taifa Israeli mtumishi wangu;sikiliza ewe kizazi cha Yakobo mteule wangu.

2. Mimi, Mwenyezi-Mungu Muumba wako,niliyekufanya tangu tumboni mwa mama yako,nimekuja kukusaidia wewe.Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:Usiogope, ewe taifa la Yakobo, mtumishi wangu,naam, usiogope ewe Yeshuruni mteule wangu.

3. “Nitaimwagilia maji nchi iliyokauka,na kutiririsha mto katika nchi kame.Nitawamiminia roho yangu wazawa wako,nitawamwagia watoto wako baraka yangu.

4. Watachipua kama nyasi penye maji mengi,kama majani kandokando ya vijito.

5. “Mmoja atasema: ‘Mimi ni wa Mwenyezi-Mungu’,mwingine atajiita kwa jina la Yakobo,mwingine ataandika mkononi mwake, ‘Wa Mwenyezi-Mungu’,na kujitambulisha kwa jina la Israeli.”

Isaya 44