19. Tazameni, mimi ninafanya kitu kipya.Kinafanyika sasa hivi,nanyi mtaweza kukiona.Nitafanya njia nyikani,na kububujisha mito jangwani.
20. Wanyama wa porini wataniheshimu,kina mbweha na kina mbuni,maana nitaweka maji nyikani,na kububujisha mito jangwani,ili kuwanywesha watu wangu wateule,
21. watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe,ili wazitangaze sifa zangu!’
22. “Lakini ewe taifa la Yakobo, hukuniabudu mimi;enyi watu wa Israeli, mlinichoka mimi!