26. Nani aliyebashiri haya tangu mwanzo,hata sisi tupate kuyatambua?Nani aliyetangulia kuyatangaza,ili sasa tuseme, alisema ukweli?Hakuna hata mmoja wenu aliyeyataja,wala hakuna aliyesikia maneno yenu.
27. Mimi ni yule wa kwanza, niliyetangaza kwa Siyoni,nikapeleka Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
28. Nimeangalia kwa makini sana,lakini simwoni yeyote yule;hamna yeyote kati ya hao miungu awezaye kushauri;nikiuliza hakuna awezaye kunijibu.
29. La! Miungu hiyo yote ni udanganyifu,haiwezi kufanya chochote;sanamu zao za kusubu ni upuuzi.