Isaya 33:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ole wako ewe mwangamizi,unayeangamiza bila wewe kuangamizwa!Ole wako wewe mtenda hila,ambaye hakuna aliyekutendea hila!Utakapokwisha kuangamizawewe utaangamizwa!Utakapomaliza kuwatendea watu hilawewe utatendewa hila.

2. Ee Mwenyezi-Mungu, utuonee huruma,kwako tumeliweka tumaini letu.Uwe kinga yetu kila siku,wokovu wetu wakati wa taabu.

3. Kwa kishindo cha sauti yako watu hukimbia;unapoinuka tu, mataifa hutawanyika.

4. Maadui zao wanakusanya mateka,wanayarukia kama panzi.

Isaya 33