Isaya 31:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ole wao wale waendao Misri kuomba msaada,ole wao wanaotegemea farasi,wanaotegemea wingi wa magari yao ya vita,na nguvu za askari wao wapandafarasi,nao hawamtegemei Mtakatifu wa Israeli,wala hawamwombi Mwenyezi-Mungu shauri!

2. Mungu ni mwenye busara na huleta maangamizi.Habadilishi tamko lake;ila yuko tayari kuwakabili watu waovukadhalika na wasaidizi wa watendao mabaya.

3. Wamisri ni binadamu tu wala si Mungu;farasi wao nao ni wanyama tu, si roho.Mwenyezi-Mungu akiunyosha mkono wake,taifa linalotoa msaada litajikwaa,na lile linalosaidiwa litaanguka;yote mawili yataangamia pamoja.

Isaya 31