Isaya 28:9-11 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Wao wananidhihaki na kuuliza:“Huyu nabii ataka kumfundisha nani?Je, anadhani atatueleza sisi ujumbe wake?Je, sisi ni watoto wachangawalioachishwa kunyonya juzijuzi?

10. Anatufundisha kama watoto wadogo:Sheria baada ya sheria,mstari baada ya mstari;mara hiki, mara kile!”

11. Haya basi!Mwenyezi-Mungu ataongea na watu hawakwa njia ya watu wa lugha tofautiwanaoongea lugha ngeni.

Isaya 28