Isaya 16:10-12 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Furaha na shangwe zimetoweka katika shamba la rutuba.Kwenye mizabibu hakuna kuimba tena,wala kupiga vigelegele.Hakuna tena kukamua zabibu shinikizoni,sauti za furaha za mavuno zimekomeshwa.

11. Hivyo, nafsi yangu yalilia Moabu kama kinubi,na moyo wangu kwa ajili ya mji wa Kir-heresi.

12. Watu wa Moabu wanapojitokeza kuabudu mungu wao,wanapojichosha huko juu mahali pa ibada,wanapokwenda mahali pao patakatifu kusali,hawatakubaliwa.

Isaya 16