Isaya 14:8-11 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Misonobari inafurahia kuanguka kwako,nayo mierezi ya Lebanoni pamoja yasema:‘Kwa vile sasa umeangushwa,hakuna mkata miti atakayekuja dhidi yetu!’

9. “Kuzimu nako kumechangamka,ili kukulaki wakati utakapokuja.Kunaiamsha mizimu ije kukusalimuna wote waliokuwa wakuu wa dunia;huwaamsha kutoka viti vyao vya enziwote waliokuwa wafalme wa mataifa.

10. Wote kwa pamoja watakuambia:‘Nawe pia umedhoofika kama sisi!Umekuwa kama sisi wenyewe!

11. Fahari yako imeteremshwa kuzimupamoja na muziki wa vinubi vyako.Chini mabuu ndio kitanda chako,na wadudu ndio blanketi lako!’

Isaya 14