8. Misonobari inafurahia kuanguka kwako,nayo mierezi ya Lebanoni pamoja yasema:‘Kwa vile sasa umeangushwa,hakuna mkata miti atakayekuja dhidi yetu!’
9. “Kuzimu nako kumechangamka,ili kukulaki wakati utakapokuja.Kunaiamsha mizimu ije kukusalimuna wote waliokuwa wakuu wa dunia;huwaamsha kutoka viti vyao vya enziwote waliokuwa wafalme wa mataifa.
10. Wote kwa pamoja watakuambia:‘Nawe pia umedhoofika kama sisi!Umekuwa kama sisi wenyewe!
11. Fahari yako imeteremshwa kuzimupamoja na muziki wa vinubi vyako.Chini mabuu ndio kitanda chako,na wadudu ndio blanketi lako!’