7. Lakini Ashuru hakudhamiria hivyo,yeye alikuwa na nia nyingine;alikusudia kuharibu kabisa,kuangamiza mataifa mengi iwezekanavyo.
8. Maana alisema:“Je, si kweli majemadari wangu ni wafalme?
9. Je, si kweli kwamba Kalno nitautenda kama Karkemishi,mji wa Hamathi kama mji wa Arpadi,Samaria kama Damasko?
10. Kama nimefaulu kuunyosha mkono wangudhidi ya falme zenye sanamu za miungukubwa kuliko sanamu za Yerusalemu na Samaria;
11. je, nitashindwa kuutenda Yerusalemu na sanamu zake,kama nilivyoutenda Samaria na sanamu zake?”
12. Wakati Mwenyezi-Mungu atakapomaliza kazi zake zote mlimani Siyoni na mjini Yerusalemu, atamwadhibu mfalme wa Ashuru, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.