Isaya 10:17-25 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Mungu aliye mwanga wa Israeli atakuwa kama moto,Mtakatifu wa Israeli atakuwa mwali wa motoambao kwa siku moja utateketeza kila kitu:Miiba yake na mbigili zake pamoja.

18. Misitu yake ya fahari na mashamba yake mazuri,Mwenyezi-Mungu atayaangamiza yote;itakuwa kama mtu aliyemalizwa na ugonjwa.

19. Miti itakayobaki msituni mwake itakuwa michache sanahata mtoto mdogo ataweza kuihesabu.

20. Siku ile wazawa wa Yakobo watakaobaki, naam, Waisraeli watakaosalia hawatalitegemea tena taifa lililowaadhibu, bali watamtegemea kabisa Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli.

21. Wazawa wa Yakobo wachache watakaobaki watamrudia Mungu Mkuu.

22. Maana, hata kama sasa Waisraeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaorudi. Maangamizi yamepangwa yafanyike, nayo yatafanyika kwa haki tupu.

23. Naam! Bwana, Mwenyezi-Mungu wa majeshi, atakamilisha kabisa katika nchi yote jambo aliloamua kutenda.

24. Kwa hiyo, Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Enyi watu wangu mnaokaa Siyoni msiwaogope Waashuru ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua mikongojo yao dhidi yenu kama walivyofanya Wamisri.

25. Maana bado kitambo, nayo hasira yangu itapita na ghadhabu yangu itawageukia Waashuru.

Isaya 10