1. Waefraimu waliponena, watu walitetemeka;Waefraimu walikuwa na uwezo mkubwa huko Israeli,lakini walianza kumwabudu Baali, wakajiletea kifo.
2. Waefraimu wameendelea kutenda dhambi,wakajitengenezea sanamu za kusubu,sanamu zilizotengenezwa kwa ustadi wao,zote zikiwa kazi ya mafundi.Wanasema, “Haya zitambikieni!”Wanaume wanabusu ndama!