7. Watu wangu wamepania kuniacha mimi,wakiitwa waje juu,hakuna hata mmoja anayeweza.
8. Ewe Efraimu, nawezaje kukuacha?Nawezaje kukutupa ewe Israeli?Nitawezaje kukufanya kama mji wa Adma?Nitawezaje kukutenda kama Seboimu!Nazuiwa na moyo wangu;huruma yangu imezidi kuwa motomoto.
9. Nitaizuia hasira yangu kali;sitamwangamiza tena Efraimu,maana mimi ni Mungu, wala si binadamu.“Mimi ndimi Mtakatifu miongoni mwenu,nami sitakuja kuwaangamiza.
10. “Watanifuata mimi Mwenyezi-Mungu ningurumaye kama simba;nitakaponguruma watanijia toka magharibi wakitetemeka.
11. Watakuja kutoka Misri wakitetemeka kama ndege,wataruka kutoka Ashuru kama huanami nitawarudisha makwao;mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
12. Watu wa Efraimu wananirundikia uongo,na Waisraeli udanganyifu.Watu wa Yuda, wananiasi mimi Mungu Mtakatifu.