5. Basi, Waisraeli waliondoka Ramesesi, wakapiga kambi yao huko Sukothi.
6. Kutoka Sukothi, walipiga kambi yao huko Ethamu, ukingoni mwa jangwa.
7. Kutoka Ethamu, waligeuka na kurudi hadi Pi-hahirothi, mashariki ya Baal-sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8. Waliondoka Pi-hahirothi, wakapita bahari ya Shamu mpaka jangwa la Ethamu; walisafiri jangwani mwendo wa siku tatu, wakapiga kambi yao Mara.
9. Kutoka Mara, walisafiri hadi Elimu; huko Elimu kulikuwa na chemchemi kumi na mbili za maji na mitende sabini, wakapiga kambi yao mahali hapo.
10. Walisafiri kutoka Elimu, wakapiga kambi yao karibu na bahari ya Shamu.