Hesabu 3:16-22 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Basi, Mose akawahesabu kufuatana na neno la Mwenyezi-Mungu, kama alivyomwamuru.

17. Wafuatao ndio waliokuwa wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.

18. Na haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni kwa kufuata familia zao: Libni na Shimei.

19. Wana wa Kohathi kwa kufuata familia zao: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.

20. Wana wa Merari kwa kufuata familia zao: Mahli na Mushi. Hizi zilikuwa jamaa za Walawi kulingana na koo zao.

21. Familia za Walibni na Washimei zilitokana na Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa jamaa za Wagershoni.

22. Idadi yao kwa kadiri ya hesabu ya wanaume wote kuanzia waliokuwa na mwezi mmoja na zaidi ni 7,500.

Hesabu 3