16. Basi, Mose akawahesabu kufuatana na neno la Mwenyezi-Mungu, kama alivyomwamuru.
17. Wafuatao ndio waliokuwa wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
18. Na haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni kwa kufuata familia zao: Libni na Shimei.
19. Wana wa Kohathi kwa kufuata familia zao: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
20. Wana wa Merari kwa kufuata familia zao: Mahli na Mushi. Hizi zilikuwa jamaa za Walawi kulingana na koo zao.
21. Familia za Walibni na Washimei zilitokana na Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa jamaa za Wagershoni.
22. Idadi yao kwa kadiri ya hesabu ya wanaume wote kuanzia waliokuwa na mwezi mmoja na zaidi ni 7,500.