Hesabu 26:49-54 Biblia Habari Njema (BHN)

49. Yeseri na Shilemu.

50. Hizi ndizo koo za kabila la Naftali, jumla wanaume 45,400.

51. Idadi ya wanaume Waisraeli waliohesabiwa ilikuwa 601,730.

52. Kisha Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose,

53. “Makabila haya yatagawiwa nchi iwe urithi wao, kulingana na idadi ya majina yao.

54. Kabila kubwa litapewa sehemu yao kubwa na dogo litapewa sehemu yao ndogo. Kila kabila litapewa urithi wake kulingana na idadi ya watu wake.

Hesabu 26