8. na kumfuatia yule Mwisraeli mpaka hemani, akawachoma mkuki wote wawili tumboni. Maradhi mabaya yaliyokuwa yamewaangamiza Waisraeli yakakomeshwa.
9. Waliokufa kutokana na maradhi yale mabaya walikuwa watu 24,000.
10. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,
11. “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, ameizuia hasira yangu dhidi ya Waisraeli; miongoni mwenu ni yeye tu aliyeona wivu kama nilio nao mimi. Ndio maana sikuwaangamiza Waisraeli wote kwa hasira yangu.
12. Kwa hiyo mwambie kwamba ninafanya naye agano la amani.