Hesabu 2:11-16 Biblia Habari Njema (BHN)

11. kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 46,500.

12. Kisha wale watakaopiga kambi kando ya watu wa Reubeni watakuwa ni watu wa kabila la Simeoni, kiongozi wao akiwa Shelumieli mwana wa Suri-shadai,

13. kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 59,300.

14. Hatimaye kabila la Gadi, kiongozi wao akiwa Eliasafu mwana wa Reueli,

15. kikosi chake kulingana na hesabu kitakuwa na watu 45,650.

16. Jumla ya wanaume watakaokuwa katika kambi ya Reubeni kulingana na makundi yao ni watu 151,450. Hawa ndio watakaokuwa katika msafara wa pili.

Hesabu 2