16. nyinyi na yeye mtakuwa chini ya sheria ileile moja na maagizo yaleyale.”
17. Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, “Waeleze
18. Waisraeli kwamba wakati watakapoingia katika nchi ninayowapeleka
19. kila mtakapokula mazao ya nchi hiyo, mtatenga kiasi fulani na kunipa mimi Mwenyezi-Mungu.
20. Mtakapooka mikate, mkate wa kwanza wa mazao ya kwanza ya nafaka yenu utatolewa kama sadaka kutoka mahali pa kupuria nafaka.