6. Lakini sasa nguvu zimetuishia na hakuna chakula kingine isipokuwa hii mana tu!”
7. Mana ilikuwa kama punje za mtama, rangi yake ilikuwa kama ya bedoza.
8. Watu walizungukazunguka na kuikusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia au waliitwanga kwa vinu, halafu waliitokosa vyunguni na kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama ya maandazi yaliyokaangwa kwa mafuta.