4. Tena mwanamume mmoja wa kila kabila atakuwa pamoja nanyi, kila mmoja aliye kiongozi wa jamaa za kabila lake.
5. Haya ndiyo majina ya watu watakaokusaidia:Kabila la Reubeni: Elisuri, mwana wa Shedeuri;
6. Kabila la Simeoni: Shelumieli mwana wa Suri-shadai;
7. Kabila la Yuda: Nashoni mwana wa Aminadabu;
8. Kabila la Isakari: Nethaneli mwana wa Suari;
9. Kabila la Zebuluni: Eliabu mwana wa Heloni;
10. Kabila la Efraimu: Elishama mwana wa Amihudi;Kabila la Manase: Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11. Kabila la Benyamini: Abidani mwana wa Gideoni;
12. Kabila la Dani: Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13. Kabila la Asheri: Pagieli mwana wa Okrani;
14. Kabila la Gadi: Eliasafu mwana wa Deueli;
15. Kabila la Naftali: Ahira mwana wa Enani.”
16. Hawa ndio viongozi waliochaguliwa miongoni mwa jumuiya yote ya watu wa Israeli, kama viongozi wakuu wa makabila yao na viongozi wa koo za Israeli.