7. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Fikirini kama mnafanya sawa!
8. Sasa, basi, nendeni milimani mkalete miti, mlijenge upya hilo hekalu, nipate kulifurahia na kutukuzwa.
9. “Mlitazamia mavuno mengi, lakini mlipata kidogo tu. Na mlipoyaleta nyumbani, niliyapeperusha mbali. Kwa nini? Kwa sababu hekalu langu ni magofu matupu hali kila mmoja wenu anashughulikia nyumba yake.
10. Ndio maana mbingu zimeacha kunyesha mvua, nayo ardhi haioteshi mavuno.