Hagai 1:3-8 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Lakini Mwenyezi-Mungu ameniambia mimi nabii Hagai,

4. “Je, ni sawa kwenu kukaa katika majumba yenu ya fahari hali hekalu langu ni magofu matupu?”

5. Sasa, asema hivi Mwenyezi-Mungu: “Fikirini kama mnafanya sawa!

6. Nyinyi mmepanda mbegu kwa wingi, lakini mmevuna kidogo; mnakula, lakini hamshibi; mnakunywa divai, lakini hamtosheki; mnavaa nguo, lakini bado mnasikia baridi; mfanyakazi mshahara wake huwa kama umetumbukizwa katika mfuko uliotoboka.”

7. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Fikirini kama mnafanya sawa!

8. Sasa, basi, nendeni milimani mkalete miti, mlijenge upya hilo hekalu, nipate kulifurahia na kutukuzwa.

Hagai 1