7. Niliwaona watu wa Kushani wakiteseka,na watu wa Midiani wakitetemeka.
8. Ee Mwenyezi-Mungu, je, umeikasirikia mito?Je, umeyakasirikia maji ya bahari,hata ukaendesha farasi wako,na magari ya vita kupata ushindi?
9. Uliuweka tayari uta wako,ukaweka mishale yako kwenye kamba.Uliipasua ardhi kwa mito.
10. Milima ilikuona, ikanyauka;mafuriko ya maji yakapita humo.Vilindi vya bahari vilinguruma,na kurusha juu mawimbi yake.