1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:
2. “Wewe mtu! Ugeukie mlima Seiri, utoe unabii juu ya wakazi wake.
3. Uambie kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Mimi napambana nawe, ee mlima Seiri. Ninanyosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya uwe jangwa na ukiwa.