7. Mwenyezi-Mungu alinijalia tena maono mengine: Nilimwona Mwenyezi-Mungu amesimama karibu na ukuta, ameshika mkononi mwake uzi wenye timazi.
8. Naye akaniuliza: “Amosi, unaona nini?” Nikamjibu, “Naona timazi.” Kisha Mwenyezi-Mungu akasema:“Tazama! Naweka timazi kati ya watu wangu Waisraeli.Sitavumilia tena maovu yao.
9. Huko vilimani ambako wazawa wa Isaka hutambikia,kutafanywa kuwa uharibifu mtupuna maskani ya Waisraeli yatakuwa magofu.Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mfalme Yeroboamu.”