1. Ole wenu nyinyi mnaostarehe huko Siyoni,nanyi mnaojiona salama mlimani Samaria!Nyinyi mwaonekana kuwa viongozi wa taifa maarufuambao Waisraeli wote huwategemea.
2. Haya! Nendeni Kalne mkaangalie kila mahali,tokeni huko mwende hadi mji ule mkubwa wa Hamathi,kisha teremkeni hadi Gathi kwa Wafilisti.Je, falme zao si bora kuliko zenuna eneo lao si bora kuliko lenu?”
3. Nyinyi mnajaribu kuifukuza siku mbaya.Lakini mnauleta karibu utawala dhalimu.