Amosi 4:11-13 Biblia Habari Njema (BHN)

11. “Niliwaangusha baadhi yenu kwa maangamizikama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora.Wale walionusurika miongoni mwenu,walikuwa kama kijiti kilichookolewa motoni.Hata hivyo hamkunirudia.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.

12. “Kwa hiyo, enyi Waisraeli, nitawaadhibu.Na kwa kuwa nitafanya jambo hilo,kaeni tayari kuikabili hukumu yangu!”

13. Mungu ndiye aliyeifanya milima,na kuumba upepo;ndiye amjulishaye mwanadamu mawazo yake;ndiye ageuzaye mchana kuwa usiku,na kukanyaga vilele vya dunia.Mwenyezi-Mungu wa Majeshi ndilo jina lake!

Amosi 4