2 Wakorintho 3:15-18 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Naam, mpaka hivi leo kila isomwapo sheria akili zao huwa zimefunikwa.

16. Lakini, wakati mtu amgeukiapo Bwana, kifuniko hicho huondolewa.

17. Hapa “Bwana” ni Roho; na pale alipo Roho wa Bwana ndipo ulipo uhuru.

18. Basi, sisi sote ambao nyuso zetu hazikufunikwa, tunaona kama katika kioo, utukufu wa Bwana; tunabadilishwa tufanane zaidi na huo mfano wake kwa utukufu mwingi zaidi. Hiyo ni kazi yake Roho wa Bwana.

2 Wakorintho 3