2 Samueli 23:22-39 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Benaya, mwana wa Yehoyada alifanya mambo haya, akajipatia jina miongoni mwa wale mashujaa watatu.

23. Basi, akawa mashuhuri kati ya wale mashujaa thelathini, ingawa hakuwa kama wale mashujaa watatu. Na Daudi akampa cheo cha mkuu wa walinzi wake binafsi.

24. Asaheli, nduguye Yoabu, alikuwa mmoja wa mashujaa thelathini. Mashujaa wengine wa Daudi walikuwa: Elhanani, mwana wa Dodo wa Bethlehemu;

25. Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;

26. Helesi, Mpalti; Ira, mwana wa Ikeshi, Mtekoa;

27. Abiezeri, Mwanathothi; Mebunai, Mhushathi;

28. Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;

29. Helebu mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai, toka Gibea katika Benyamini;

30. Benaya, Mpirathoni; Hidai, wa vijito vya Gaashi;

31. Abialboni, Mwarbathi; Azmawethi, Mbahurimu;

32. Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani;

33. Shama, Mharari; Ahimu mwana wa Sharari, Mharari;

34. Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaaka; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;

35. Hesrawi, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;

36. Igali mwana wa Nathani, Msoba; Bani, Mgadi;

37. Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi aliyekuwa mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya;

38. Ira na Garebu, Waithri;

39. na Uria, Mhiti. Wote pamoja walikuwa mashujaa thelathini na saba.

2 Samueli 23