2 Samueli 23:2-7 Biblia Habari Njema (BHN)

2. “Roho ya Mwenyezi-Mungu imesema kwa njia yangu,aliyaweka maneno yake kinywani mwangu.

3. Mungu wa Israeli amesema,Mwamba wa Israeli ameniambia,‘Mtu anapowatawala watu kwa haki,atawalaye kwa kumcha Mungu,

4. yeye ni kama mwanga wa asubuhi,jua linapochomoza asubuhi isiyo na mawingu;naam, kama mvua inayootesha majani ardhini’.

5. Hivyo ndivyo Mungu alivyoujalia ukoo wangu.Maana amefanya nami agano la kudumu milele;agano kamili na thabiti.Naye atanifanikisha katika matakwa yangu yote.

6. Lakini wasiomcha Munguwote ni kama miiba inayotupwa tu,maana haiwezi kuchukuliwa kwa mkono;

7. kuishika, lazima kutumia chuma au mpini wa mkuki.Watu hao wataangamizwa kabisa kwa moto.”

2 Samueli 23