2 Samueli 22:38-44 Biblia Habari Njema (BHN)

38. Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza,sikurudi nyuma mpaka wameangamizwa.

39. Niliwaangamiza, nikawaangusha chiniwasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.

40. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha adui chini yangu.

41. Uliwafanya adui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.

42. Walitafuta msaada, lakini hapakuwa na wa kuwaokoa,walimlilia Mwenyezi-Mungu, lakini hakuwajibu.

43. Niliwatwanga na kuwaponda kama mavumbi ya nchi,nikawaponda na kuwakanyaga kama matope barabarani.

44. “Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu wangu,umenifanya mtawala wa mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.

2 Samueli 22