2 Samueli 22:18-22 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,aliniokoa kutoka kwa hao walionichukiamaana walikuwa na nguvu nyingi kunishinda.

19. Walinivamia nilipokuwa taabuni,lakini Mwenyezi-Mungu alikuwa kinga yangu.

20. Alinileta, akaniweka mahali pa usalama,alinisalimisha, kwani alipendezwa nami.

21. “Mwenyezi-Mungu alinipa tuzo kadiri ya uadilifu wangu;alinituza kwa vile mikono yangu haina hatia.

22. Maana, nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu,wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.

2 Samueli 22