2 Samueli 11:4-8 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Basi, Daudi alituma wajumbe wamlete. Basi Bathsheba akaja kwa Daudi, naye Daudi akalala naye; (mwanamke huyo alikuwa ndio tu amejitakasa baada ya hedhi yake); kisha akarudi nyumbani kwake.

5. Mwanamke huyo akapata mimba, naye akatuma habari kwa Daudi kuwa ana mimba yake.

6. Basi, Daudi akamtumia Yoabu ujumbe, “Mtume Uria, Mhiti kwangu.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.

7. Uria alipofika kwake, Daudi alimwuliza habari za Yoabu, watu wote, na hali ya vita.

8. Halafu Daudi alimwambia Uria, “Rudi nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Uria alitoka nyumbani kwa mfalme, na mara mfalme akampelekea zawadi.

2 Samueli 11