2 Mambo Ya Nyakati 4:19-22 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Solomoni alitengeneza vitu vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Mungu: Madhabahu ya dhahabu na meza za mikate ya kuwekwa mbele ya Mungu;

20. vinara na taa za dhahabu safi za kuangazia mahali pale patakatifu sana, kama ilivyoamriwa;

21. maua, taa na koleo, vyote vikiwa vya dhahabu safi kabisa;

22. mikasi na mabirika, visahani vya ubani na vyetezo vya kubebea moto, vyote vya dhahabu safi. Pete za hekalu za milango ya mahali pale patakatifu sana, na za milango mingine ya ukumbi, zote zilitengenezwa kwa dhahabu.

2 Mambo Ya Nyakati 4