1 Wakorintho 15:56-58 Biblia Habari Njema (BHN)

56. Kifo hupata sumu yake katika dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika sheria.

57. Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.

58. Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.

1 Wakorintho 15