1 Wakorintho 13:3-7 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Nikitoa mali yangu yote na kuwapa maskini, na tena nikiutoa mwili wangu uchomwe, kama sina upendo hiyo hainifai chochote.

4. Mwenye upendo huvumilia, hufadhili; mwenye upendo hana wivu, hajidai, wala hajivuni.

5. Mwenye upendo hakosi adabu, hatafuti faida yake binafsi, wala hana wepesi wa hasira; haweki kumbukumbu ya mabaya,

6. hafurahii uovu, bali hufurahia ukweli.

7. Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, na hustahimili yote.

1 Wakorintho 13