1 Wakorintho 10:25-27 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;

26. maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”

27. Kama mtu ambaye si mwaamini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.

1 Wakorintho 10